Tuesday, September 13, 2011

Villa squad vs Azam leo Chamazi

Katibu wa Villa Iddy Godigodi




Leo Septemba 13 Vijana machachari wa timu ya Soka ya Villa Squad wanatarajia kushuka dimbani kumenyana na wenyeji wao timu ya Azam FC, katika dimba hilo lililopo nje ya mji, Chamazi.  Mchezo huo utakua ni wa tano wa ligi kuu  ya Tanzania Bara..'VPL 2011-2012..


Bila shaka Vijana wa Villa Squad ambao walitoka kujeruhiwa goli moja katika mchezo wao ulipigwa mjini Tanga, uwanja wa Mkwakwani na kwa kufungwa bao 1, na Simba Sc, kwa mapumziko waliyopata na  mazoezi makali kutoka kwa kocha wao Abdala Msamba anayewanoa kwenye dimba la Villa lililopo viunga vya uwanja wa bonde la Jangwani.


Kikosi kamili cha Villa kimejiandaa vya kutosha kuakikisha wanaibuka na ushindi wa kishindo kwani wamedhamiria kufuta makosa yao katika mchezo huo hasa kutokana na kosa la mlinzi wao hata hivyo limefanyiwa kazi na watahakikisha wanaibuka na ushindi mnono.


"Leo ni lazima tufanye kile tulichofundishwa na kuakikisha Villa inafanya vizuri na kuzima ngebe za wapinzani wetu," alisema nahodha wa timu hiyo Shai Mpala.


Mpala pia alisema watahakikisha wanafanyia kazi mafundisho ya kocha na kuakikisha waleta ushindi dhidi ya Azam ambao mchezo wao wa juzi walitoka sare ya bila kufungana na Simba Sc.


Kwa upande wake Katibu mkuu wa timu hiyo Iddy GodiGodi alisema kikosi kipo imara na kinaendelea vizuri na hakuna majeruhi na pamoja uongozi umejiandaa kukabiriana kwa jambo lolote katika kuakikisha Villa inakua imara


(Imeandikwa na Afisa Habari wa Villa, Andrew Chale 0719076376,





0 comments:

Post a Comment